GREDI YA 6 KISWAHILI APRILI 2024…

GRADE 8 ENGLISH ASSIGNMENT APRIL 2024
April 11, 2024
GRADE 8 AUGUST 2024 ASSIGNMENT
June 26, 2024

GREDI YA 6 KISWAHILI APRILI 2024…

Welcome to your GREDI YA 6 KISWAHILI APRILI 2024...

GREDI YA 6.  KAZI YA LIKIZO, APRILI 2024

SHUGHULI A KISWAHILI

MAJADILIANO

VIUNGO VYA MAPISHI
Je, unaweza kuvitambua viungo hivi vya mapishi katika picha hii?



Soma majadiliano haya baina ya mama na mtoto wake kisha ujibu maswali.
MTOTO: Shikamoo mama.
MAMA: Marahaba mwanangu, umeshindaje?
MTOTO: Nimeshinda vyema mama. Shuleni tumesoma mengi.
MAMA: Ahsante mwanangu. Jitahidi! Jitahidi sana!
MTOTO: Mama, mwalimu wetu wa Kiswahili ametupa kazi ya kuvijua viungo vya mapishi. Amesema tusaidiwe na wazazi.
MAMA: Sawa, chukua kitabu basi uandike.
MTOTO: Ahsante mama. Niko tayari.
MAMA: Tutaanza kwa kitunguu. Kuna kitunguu maji, kitunguu viazi na kitunguu thumu ama saumu. Pia kuna pilipili za aina nyingi. Kuna kichaa, pilipili manga, pilipili boga na pilipili za kawaida.
MTOTO: Pilipil hoho ni gani mama?
MAMA: Pilipili hoho ni ndogo ambazo huwa kali zaidi. Nazo pilipili boga huwa kubwa, mara nyingi za kijani wala si kali hata kidogo.
MTOTO: Mama hizo kubwa ndizo huitwa hoho.
MAMA: Hapana mwanangu. Hayo ni makosa. Hoho ni kali sana na ndogo kabisa.
MTOTO: Mwalimu alisema kuna tangawizi. Hiyo ni nini?
MAMA: Tangawizi ni kiungo kitachotiwa katika chai au chakula. Huwa kinasababisha ladha tamu na ni dawa pia. Pia kuna ndimu. jira, nyanya, bamia, halwaridi ya chai, kuna bizari, iliki, karafuu, mdalasini na masala. Viungo ni vingi mwanangu.
MTOTO: Mama unajua vingine? Nataka kujua zaidi. Mwalimu wetu anapenda wanafunzi wanaojitahidi sana kufanya kazi ya ziada.
MAMA: Aah! Vilevile kuna manjano, kungumanga, zabibu kavu, mrihani, giligiliani hata uwatu.
MTOTO: (Akicheka sana)Mama manjano ni rangi si kiungo cha chakula.
MAMA: Pia ni kiungo cha chakula ambacho wazungu huita tumeric. Ni kizuri sana kwa kusafisha damu na kutunza figo.
MTOTO: Aah! Kumbe mama unajua viungo vingi hivyo! Ahsante sana kwa kunisaidia. Mwalimu wetu atafurahi sana.
Hewala mwanangu. Sasa acha nikanunue dania nayo nipikie mchuzi.

MANENO MAPYA.
Tumia kamusi yako utafute maana ya maneno haya.
  • tangawizi
  • mdalasini
  • iliki
  • karafuu
  • jira
  • giligiliani
  • manga
  • kungumanga
  • hoho
Jibu maswali haya.
1. Ni kiungo kipi kati ya hivi utatia katika chai?

2. Ni pilipili gani kati ya hizi ambayo si kali?

3. Karafuu hukuzwa zaidi katika nchi gani?

4. Ni nini kati ya vitu hivi si kiungo cha chakula?

5. Masala hutumiwa sana kupikia wali wa ___

6. Halwaridi hutumiwa zaidi katika kupikia __

7. Kando na kutia ladha katika chakula baadhi ya viungo hutumika kama ______

8. Kulingana na majadiliano uliyosoma, tunawea kusema kuwa mama _____

9. Mtoto huyu anaonyesha kuwa _

10. Mtu anapokwambia ahsante, unafaa kujibu namna gani?

B. MATUMIZI YA LUGHA

UKOO AU NASABA.
Ukoo ni uhusiano wa kidamu wa watu.Ukoo hujumlisha watu waliozaliwa na mtu mmoja au waliotoka familia tofauti lakini wakaunganishwa na ndoa.Tazama mifano hii:

  • Babu na nyanya/bibi - wazazi wa wazazi wako.
  • Ami/amu - kaka yake baba
  • Shangazi/mbiomba - dada yake baba
  • Mjomba/hau - kaka yake mama
  • Halati/hale - dada yake mama
  • Binamu/mkoi - mtoto wa mjomba, shangazi, ami au hale.
  • Mpwa - mtoto wa ndugu yako
  • Umbu - jina la kuitana baina ya kaka na dada
  • Mnuna - ndugu yako mdogo awe wa kiume au kike
  • Mlungizi - ndugu anayekufuata katika kuzaliwa
  • Mwanambee/kifungua mimba - mtoto wa kwanza kuzaliwa
  • Kichinjamimba/kifungamimba - mtoto wa mwisho kuzaaliwa
  • Wifi - jina la kuitana baina ya mke na dada yake mume wake
  • Mwamu/mlamu - jina la kuitana baina ya mume na kaka yake mke wake
  • Mwanyumba - Wanaume waliooa kutoka familia moja
  • Mkazahau - mke wa mjomba
  • Shemeji/shemegi - jina la kuitana baina ya mume au mke na ndugu wa mke au mume ambaye ni ambaye ni wa jinsia tofauti.

1. Watu wenye uhusiano wa kidamu huitwaje_______

12. Dada yake mama huitwaje?

13. Mke wa mjomba huitwaje?

14. Dada yake baba huitwaje?

15. Wanaume wawili walioa kina dada wa familia moja huitanaje?

16. Mtoto wa kwanza kuzaliwa huitwaje?

17. Mtoto wa mwisho kuzaliwa huitwaje?

18. Mama yake mama huitwaje?

19. Mtoto mdogo sana huitwaje?

20. Wanawake wawili walioolewa na mwanamume mmoja huitanaje?

Katika maswali yafuatayo, chagua aina ya kivumishi kilichopigiwa mstari kutoka katika orodha uliyopewa hapa.

idadi, kimilikishi, kiashiria, sifa, pekee.

1. Musa amenunua kalamu nzuri dukani.

22. Wanafunzi watakaoenda ziara ya Amboseli watakuwa tisini na wawili.

23. Watoto wote wamepata chanjo sasa, itawazuia kupata ugonjwa wa ukambi.

24.  Nina furaha kwa sababu shule yetu inatufunza matumizi ya teknolojia.

25. Mti uliokatwa ulikuwa mahali pale.

Tumia kirejeshi amba kwa usahihi kukamilishia sentensi zifuatazo.

26. Mama amebeba mfuko __________ ulinunuliwa jana.

27. Kanisa _______ huwaibia waumini wake hufungwa.

28. Wakati ________ tetemeko lilisikika nilikuwa nikiota.

29. Mzazi __________ atafika mkutanoni akiwa wa kwanza atatuzwa

30. Huko _______ wamesimama kuna siafu.

KUWA NA LIVU NJEMA YA FURAHA

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WeCreativez WhatsApp Support
One of our Teachers is here. Ask for help
Hi, how can I help