HYGIENE & NUTRITION GRADE 3.June 20, 2020STD 7 S/STJune 22, 2020 0 KISWAHILI 8. Welcome to your KISWAHILI 8. SOMO LA KISWAHILIKAULI YA KUTENDESHATazama picha hii. Mwalimu anafanya nini?Kauli ya kutendesha huonesha mtu akifanya mtu mwengine afanye jambo, au kitu kikifanya kingine kifanye jambo. Katika picha hii, mwalimu anawafanya wanafunzi wasome, kwa hivyo anawasomesha.Kauli ya kutendesha ina jinsi sita kama ifuatavyo:1. Kitenzi huishia kwa -sha soma - somesha pika - pikisha andika - andikisha2. Kitenzi huishia kwa -za fanya - fanyiza penda - pendeza oa - oza3. Kitenzi hushia kwa -vya lewa - levya nawa - navya lowa - lovya4. Kitenzi huishia kwa -fya ogopa - ogofya ongopa - ongofya5. Kitenzi huishia kwa -sa tokota - tokosa nata - nasa 6. Kitenzi huishia kwa -nya gawana - gawanya pona - ponya MASWALI.Jaza mapengo katika sentensi hizi kwa kutumia kitenzi katika kauli ya kutendesha.1. Siti Maria alim_____ mtoto kitandani alipolia. lalisha laza lavya None 2. Wazee wamekanywa kuwa______ binti zao wakiwa wadogo. oa olesha oza None 3. Ni vizuri kuwa_______ watu umuhimu wa masomo. juza julisha jufya None 4. Mama alim_______ mwanawe mti kwa shoka butu. katiza katisha katisa None 5. Ni nani alim______ paka wetu majini? toza tosha tosa None 6. Si vizuri kum_______mnyama yeyote. fiza fisha fifya None 7. Mwalimu alitu______ kulaza damu darasani. kanisha kanya kanisa None 8. Mbwa wa Thuranira wana________ sana. ogopesha ogopeza ogofya None 9. Pombe _______ hulewesha hulevya huleweza None 10. Mwanaskauti ame_______ bendera vizuri. pandisa pandisha pandiza None Time's up Wanto Leave a Reply Cancel replyYour email address will not be published. Required fields are marked *Comment * Name * Email * Website Save my name, email, and website in this browser for the next time I comment. Δ