Welcome to your KISWAHILI 8,,
KISWAHILI DARASA LA 8SOMO : KAULI YA KUTENDEKA.Tazama picha hizi.(i) Huyu ni mzee Thuranira. Mzee Thuranira amelima shamba lake ili apande viazi. Shamba hili limelimwa likalimika. (ii) Huyu ni mam Sein. Mama Sein amepika chakula kitamu sana. Chakula kimepikwa kikapikika.Kauli ya kutendeka huonyesha kuwa kitendo kimefanyika. Kwa hivyo ni lazima kitendo kiwe kimefanywa ili nacho kifanyike. Ikiwa kitendo huishia kwa irabu au vokali (a,e,i,o,u) mnyambuliko wa kitendo hicho hubadilika na kuongezea l. Hapa pana mifano miwili ya minyambuliko hiyo. Ai) lima - limikaii) pika - pikikaiii) piga - pigikaiv) osha - oshekav) imba - imbika Bi) tia - tilikaii) oa - olekaiii) lea - lelekaiv) tii - tiilikav) pokea - pokeleka.JIBU MASWALI HAYA KWA KAULI IFAAYO YA KUTENDEKA.1. Kemboi alikimbia mbio za masafa marefu___
2. Yusuf amekunywa maziwa ______
3. Mama Aisha amefua nguo _____
4. Mtoto alimuua mdudu _____
5. Githiga hucheza soka hadi _____
6. Askari walimtoa mwizi mbio mpaka ______
7. Tumesoma Kiswahili _____
8. Mwalimu Mwasimba alilighani shairi hadi ____
9. Ni vuzuri kufanya kazi vizuri hadi______
10. Jogoo aliwika hadi _____
Time's up
Your email address will not be published. Required fields are marked *
Comment *
Name *
Email *
Website
Save my name, email, and website in this browser for the next time I comment.
Δ