KISWAHILI 6September 16, 2020STD 6 ENGLISHSeptember 17, 2020 0 KISWAHILI 8 Welcome to your KISWAHILI 8 Name Class Phone KISWAHILI DARASA LA 8.MADA: SARUFIMADA NDOGO: Mkato wa maneno yenye Sauti nne.Huyu ni Mama Kasioki. Mama Kasioki anavuna mboga za majani katika shamba lake. Shambale ni kubwa sana. Anataka kupika ugali ale na wana wake. Wanawe wakimaliza kula wataenda kucheza. Mama naye atavua kanga yake ili aifue. Kangaye ikikauka, atajifunga tena. Watoto wasipocheza vizuri wataumizana. Kweli asiyefunzwa na mamaye hufunzwa na ulimengu.Maneno yaliyo angaziwa ni mkato wa maneno yenye sauti nne. Shamba lake - shambale Mama yake - mamaye Kanga yake - kangaye Wana wake - wanawe Katika kukata sauti nne, onatoa sauti mbili za katikati kisha unaunganisha mbili zinazobaki. Kwa mfano Kalamu Yake - kalamuye Gari lake - garile. Hata hivyo, kimilikishi wako hukatwo na kubaki o pekee. Mwana wako - mwanao. NB: Vimilikishi vyenye maneno matatu havifupishwi. Mfano yao pao lao - hubaki vivyo hivyo. MASWALI. Fupisha maneno yaliyoangaziwa katika sentensi.1. Baba yake Juma ni kandawala. 2. Kila mwanafunzwi anafaa kukaa pahali pake. 3. Mari na dada zake wameenda mtoni. 4. Kesho ukienda kwa babu yako umsalimu sana. 5. Naona kama nguo zako zote hutoka India. 6. Maisha yako unayatakiaje? 7. Wazee wanaooza binti zao wadogo watatiwa ndani. 8. Mbona mwana wako hapendi ushauri? 9. Maseremala hawajamaliza kuunda meza zake Ali. 10. Mwana wao hajaoenekana tangu juzi. Time's up Wanto Leave a Reply Cancel replyYour email address will not be published. Required fields are marked *Comment * Name * Email * Website Save my name, email, and website in this browser for the next time I comment. Δ