STD 7 ENGLISH PART II.April 8, 2021GREDI YA 4 KISWAHILI. 2024 MID-TERM 2April 10, 2021 0 KISWAHILI DARASA LA 7 Welcome to your KISWAHILI DARASA LA 7 Name Class Phone ZIADA YA LIKIZO YA APRILI 2021, DARASA LA 7.LET US TAKE A MINUTE AND CONGRATULATE OUR CLASS 8 2020 FOR GOOD PERFORMANCE. WELL DONE.408405403383374370370365362359357355355351.......The list continues........33 Over 300 marks. We thank God. KISWAHILI. MADA: KUSOMA NA KUFAHAMIKIWA SOMO UFAHAMU. Tazama picha hii. Unafikiria ni shughuli gani inayoendelea?Je, shule yenu ishawahi kushiriki katika shughuli kama hii?SOMA UFAHAMU UFUATAO Ilikuwa siku ya matembezi ya kukusanya pesa kwa ajili ya wagonjwa wa maradhi sugu yasiyopona.Wanafunzi wa shule ya upili ya Kiria-ini ambao walikuwa wamejisajili kwa shughuli hiyo walijitayarisha mapema. Walikuwa watembee mwendo wa kilometa nane kutoka shuleni kisha warudi kuko huko. Hii iliwabidi kutoka mapema yapata mwendo wa saa tatu asubuhi. Takriban wanafunzi themanini ndio waliopata nafasi. Lulu na Nikko walikuwa miongoni mwao. Matembezi hayo yalisimamiwa na walimu wanne; wawili wa kike na wawili wa kiume. Bi. Neema alikuwa mmoja wao. Baada ya kupewa mashauri na kuelekezwa kuhusu matembezi hayo, wote waliondoka shuleni kwa pamoja wakielekea kituoni ambapo walipewa fulana zenye maandishi kuhusu matembezi hayo. Kutoka hapo walitembea pamoja hadi walipoanza kufumukana kwa makundi makundi. Wale waliokuwa wepesi waliongoza wengine huku watepetevu wa kutembea wakisumbukia hali zao. Jua la mtikati liliwapata taraa walipowasili kwenye kituo cha mwisho ili wageuke waanze kurudi.Hapo ilikuwa watue kwa muda ili kupokea hotuba ya naibu wa waziri wa afya kabla hawajarudi. Wahudumu waliokuwapo kwenye kituo hicho waliwahudumia kwa maji safi pamoja na sharubati angaa wakonge roho. Kwa wale waliolilia dawa za kuwangwa na kichwa, walipewa vidonge vya kutuliza hali hiyo. Baada ya hotuba fupi kutolewa, wanafunzi waliketi pamoja ili wapewe chamcha.Walimu wawili waliwachukua wanafunzi kadhaa ambao waliwaauni kubeba vilaji. Bila shaka chakula chepesi ni soda na mkate. Aidha kila mmoja aliongezewa yai la kutokoswa na ndizi moja ya mkono wa tembo. Wakati wakila, Lulu alihama pahali alipoketi na kujiunga na kikundi ambapo Nikko alikuwa. Kilikuwa kikundi cha wavulana watano. Watatu walipomuona waliona izara wakagura kutoka hapo. Nikko alimpokea Lulu wakala pamoja huku wakibadilishana mawazo. Lulu aliamlaumu Nikko kwa kutotembea pamoja naye, naye akajitetea akisema hakupata fursa ya kumuita. Waliahidiana kuwa watakuwa pamoja wakirudi shuleni. Mengi hayakujiri hapo kwani walikuwa sehemu wazi na walimu walikuwa macho sana. Bi Neema hakumaliza zaidi ya dakika tano pasipo kumgeukia Nikko. Pamoja na hayo, wanafunzi wengine walikuwa ange kusikiliza udaku wa wenzi wao na dondoo za mjini. -Kutoka kitabu 'Mchezo Wa Wanawake' na Wanto Warui.A. MSAMIATI.Tumia Kamusi yako kutafuta maana ya maneno haya: sajili bidi takriban shauri fulana fumukana ~tepetevu mtikati taraa tua hudumu sharubati konga wanga kidonge chamcha auni kilaji tokosa izara gura fursa jiri ange udaku dondoo. JIBU MASWALI YAFUATAYO:1. Kulingana na aya ya kwanza, _____________ matembezi yalikuwa ya kukusanya pesa za kutibu maradhi pesa ambazo zingekusanywa katika matembezi zingesaidia kutibu maradhi sugu wagonjwa wa maradhi sugu wangesaidika kuongeza maisha kupitia pesa za matembezi pesa ambazo zingekusanywa zingetumika kujenga hospitali ya kutibia wagonjwa. None 2. Wanafunzi wa Shule ya Upili ya Kiria-ini wangetembea kwa urefu gani? Kilometa nane Kilometa nne kilometa kumi na sita kilometa kumi na nne None 3. Ni wanafunzi wangapi wa shule ya Kiria-ini walikuwa wamejiandikisha katika matembezi? sabini na wanane themanini thelathini thelathini na wanane None 4. Mmojawapo wa walimu waliosimamia matembezi hayo alikuwa ni ______ Lulu Nikko Mwalimumkuu Bi. Neema None 5. Wanafunzi walianza kufumukana kwa makundi _________ pindi walipoanza kuchoka ili waweze kutembea haraka ili waweze kujadili mambo ya matembezi hayo walipoona walimu wao hawana shughuli nao None 6. Ni mwendo wa saa ngapi ambapo wanafunzi waliweza kuwasili kituoni walipotolewa hotuba? alfajiri adhuhuri alasiri mawio None 7. Kukonga roho kama lilivyotumika katika kifungu lina maana ya___ kuongeza kiu kusababisha kiu ya maji kupunguza njaa kuondoa nyota None 8. Chakula cha mchana walichokula wanafunzi kilikuwa____ soda,chapati, ndizi, yai yai,soda, mkate,embe tembo, ndizi, mkate, soda soda, mkate, yai, ndizi None 9. Kulingana na kifungu _____ Lulu na Nikko walikuwa mahasidi Lulu na Nikko walienziana Lulu na Nikko walikuwa walimu Lulu na Nikko walikuwa maadui None 10. "Wale waliokuwa wepesi waliongoza wengine huku watepetevu wa kutembea wakisumbukia hali zao."Ni methali gani inayoweza kutumiwa kuelezea maneno haya? Ndovu hashindwi na mkongawe Kila mwamba ngoma ngozi huivuta na kwake Mgaagaa na upwa hali wali mkavu Safari ya mbali huanza kwa hatua None Tumia maneno ya msamiati uliyosoma hapo juu kujalizia mapengo haya:Mwalimu wetu alitwambia tufanye kazi kwa bidii hapendi wanafunzi_______ wahudumu watepetevu wakonga None 12. Watoto waliofikisha umri wa miaka minne wanafaa _______ shuleni. kuauniwa kusajiliwa kuadhibiwa None 13. Ni vizuri kumeza ______ punde tu kichwa kinapo______. auni, fumukana taraa, bidi vidonge, wanga None 14 Wakati wa saa saba mchana huwa tunakula_____ chajio izara chamcha None 15. Wanaume wengi hawapendi wanawake wenye _____ dondoo udaku auni None Chakula cha pure hupikwa kwa kuchanganya mahindi na maharagwe kisha ____. kutokosa kujiri kukaange None 17. Mkutano wa chifu ulipoisha, wananchi ______ walifumukana waliauana walisajiliana None 18. Wanga ni kuumwa na kichwa, wanga pia ni ______ unga wa ngano vyakula vyenye kabohaidreti kitu kipya. None 19. Baba ametupa _____ kuwa huenda rais akafungua nchi. udaku dondoo tua None 20. Askarijeshi walikaa ______ usiku kucha mji usivamiwe na magaidi. tua izara ange None B. MATUMIZI YA LUGHAChagua jibu lililo bora zaidi kkamilishia sentensi hizi:21. Fahali kwa mtamba kama vile jogoo ni kwa _____ kuku kikwara tembe koo None 22. Malipo ya kumtoa mtu damu huitwa ______ ridhaa fidia dia machorombozi None 23. Arshi ni aina ya malipo. Arshi pia ni _________ kiti anachokalia Mwenyezi Mungu mtu anayejenga kwa kutumia mawe mtu anayewachomea wengine mali yao sehemu ya ndege anapokaa rubani None 24. Chagua sentensi iliyoandikwa kwa usahihi. Ningelikuona ningelikuita Ningekuona ningalikuita Nisingekuona nisingekuita Ningalikuona ningekuita None 25. Mama atatutembeza Mombasa Jumapili.Neno lililokolezwa rangi ni ______ nomino kielezi kivumishi kiwakilishi. None 26. Chagua sentensi iliyotumia 'O' rejeshi ya mwishoni. Kitabu ambacho kilionekana ni changu Tulienda kwao ili tupewe mawaidha Mwanamuziki aimbaye vizuri hutuzwa na rais Mahali ambapo palilimwa ni pako None 27. Chagua mpangilio ufaao wa ukulima. kupanda>kupiga matuta>kuchimba makoongo>kulima. kulima>kupanda>kupalilia>kuchimba makoongo kulima>kupiga matuta>kuchimba makoongo>kupanda kuchimba>kupanda>kuvuna>kupalilia None 28. Tegua kitendawili hiki:Kutoa ni kuongeza_______ sufuria tumbo shimo kisima None 29. Kipimo cha _____ yetu hakiwezi kupimwa kwa ______. inchi, nchi inji, inchi nche, inchi nchi, inchi None 30. Wanafunzi wote waliambiwa waingie ______ wasinyeshewe. kwa kwenye ndani katika None 31. Andika milioni saba, laki saba sabini elfu na sabini kwa tarakimu. 7,770,070 7,070,070 7,700,770 7,707,070 None 32. Kifaa cha ujenzi cha kushikilia vyuma vinapokatwa ni _____ msumeno mvukuto filifil jiriwa None 33. Tumia kiunganishi mwafaka: _________ ya nchi yetu kuwa na milima ina pia mabonde. Angalau Licha Minghairi Haidhuru None 34. Sehemu ya mbele ya mkono iliyo na vidole huitwaje?______ kiwiko kitengele kikono kisugudi None 35. Chagua sehemu ya mwili iliyo tofayti na nyingine. pua ulimi mguu jicho None 36. Raia wa nchi ya Rwanda huitwaje? Warwanda Wanyarwanda Warwandese Wanyankole None 37. Mzegamzega ni mtu anayeuza maji mtaani, mtu anayefua visu ni______ mkimu mnajimu mjumu mjume None 38. Chagua sifa iliyoundwa kutokana na nomino. Kilimo - ukulima Samehe - usamehevu Ucheshi - cheshi Mlizi -liza None 39. Ni watu ______ waliokuwa hapa? yupi wagani gani mgani None 40. Ainisha maneno yaliyokolezwa katika sentensi hii.Wao walibeba mikoba mirefu kuliko wenyewe ikaanguka mtoni. kivumishi, nomino, kielezi Nomino, nomino,kivumishi Kielezi, nomino, kivumishi Kiwakilishi, kivumishi, kihusishi. None C. MTUNGO. Soma mtungo ufuatao huku ukijaliza nafasi zilizoachwa wazi kwa neno bora zaidi kati ya manne uliyopewa hapo chini. Baada ya dalili za mvua kujitokeza, wakulima walianza kujitayarisha mara moja kwa ___41_____. Walichimba ____42___ na kuyatia mbolea kisha wakapanda mbegu. Baada ya ____43____ moja, mbegu zilikuwa zimeota na ____44____. Mvua nayo ikazidi ___5____, usiku haikupusa ___46____ilinyesha mfululizo. Asilimia sabini na tano yaani ____47____wakawa wamewahi kazi zao za shambani. Wale ambao waliketi tu na ___48____ yao hawakuwa na chochote cha kula ___49____ mavuno yalipofika. Hawakujua kuwa ____50____.41. uvunaji upanzi upaliliaji unyunyiazi dawa None 42. makoongo mashimo handaki matuta None 43. mwezi mwaka juma saa None 44. kukuchuka kunyauka kuvunika kuchipuka None 45. kunya kupusa kupukutika kuanguka None 46. ! ; . : None 47. 5/10 1/4 3/4 1/3 None 48. kuyakumbatia kuikumbatia kuzikumbatia kulikumbatia None 49. kabla kitambo kisha baadaye None 50. dalili ya mvua ni mawingu! hakuna bamvua lisilokuwa na usubi! ukipanda pantosha utavuna pankwisha! ajizi ni nyumba ya njaa! None D. INSHA.Mwandikie rafiki yako barua ukimwelezea njia za kuweza kujikinga kutokana na ugonjwa wa Covid-19.AHSANTE KWA KUKAMILISHA ZIADA YAKO. UWE NA LIKIZO AJIBU.KWA HERI! None Time's up Wanto Leave a Reply Cancel replyYour email address will not be published. Required fields are marked *Comment * Name * Email * Website Save my name, email, and website in this browser for the next time I comment. Δ