GREDI YA 4 KISWAHILI. 2024 MID-TERM 2

KISWAHILI DARASA LA 7
April 9, 2021
GREDI YA 5, T1 KISWAHILI 2023.
April 10, 2021

GREDI YA 4 KISWAHILI. 2024 MID-TERM 2

Welcome to your GREDI YA 4 KISWAHILI. 2024 MID-TERM 2

ZIADA YA LIVU FUPI, KATI YA MUHULA WA 2 2024, GREDI YA 4.

ZIADA YA WAKATI HUU ITAHUSU SHUGHULI ZA KISWAHILI.

SHUGHULI ZA KISWAHILI

MAAGIZO
1. Fanya kazi yako katika MTANDAO kisha uiandike katika DAFTARI lako la kazi ya ziada.
2. Ukimaliza kufanya kazi MTANDAONI, hapo chini utaona kitufe cha kukabidhi kazi kilichoandikwa 'Submit'. Bofya na baada ya sekunde kazi yako itakuwa imesahihishwa. Tazama matokeo na ufanye marudio ya maswali uliyonoa.
3. Kumbuka utahitaji kuleta kazi iliyofanya daftarini shuleni, shule itakapofunguliwa.


SHUGHULI YA 1: KUSIKILIZA NA KUONGEA
Sikiliza kanda hii ya video kwa makini.


Tumia kamusi yako kutafuta maana ya maneno haya yaliyotumiwa katika shairi.
  •  bembea
  • tatizo
  • likizo
  • tua
  • kadhalika
  • nadhifu
  • dhaifu
  • sare
  • kwaruza
  • sindikiza
  • dekeza

Sasa jibu maswali haya:

1. Kibao kilichoning'inizwa kwa kamba mbili zilizofungiwa juu kwa ajili ya kuchezea huitwa_______

2. Ndege wakiruka huwa wana_____ mtini.

3. Muhula ukimalizika wanafunzi hupewa _____ wakapumzike.

4. Wanafunzi wote lazima wavae  _____ wakiwa shuleni.

5. Mwalimu wetu hupendeza sana kwa sababu yeye huvalia ______

6. Si vizuri wazazi ______ mtoto, ataharibika.

7. Mtu aki_______ na kijiti anaweza kutoka damu.

8. Mama alipoenda sokoni alinunua:maembe, machungwa, mboga, matofaa na _____

9. Ni ______ kubwa kukosa kumrekebisha mtoto akikosea.

10. Rafiki yako akija kwenu, ni vizuri _____ anapoenda.

11. Shairi ulilosikiliza lina beti ngapi?

12. Vina vya kati na mwisho katika ubeti wa tatu ni _______,  ________

13. Mshororo 'Kubembea kuna mambo, kubembea tunacheza' unaitwaje?____

14. "Ng'riiiiiiiiii, sasa imelizwa'. Ni nini hiyo mshairi anasema?

15. Malenga wa shairi hili ni nani?

SHUGHULI YA 2 : MATUMIZI YA LUGHA

Jibu kila swali kulingana na maagizo yake.
Toa majibu ya salamu hizi:

1. Hamjambo - ______

2. Shikamoo-______

3. Salaam aleikum - ______

Jibu vitendawili hivi:
4. Huku ng'o na kule ng'o _____________

5. Mama nieleke ______

6. Kuku wangu hutagia mibani ________

Kamilisha methali hizi:
7. Mtoto wa nyoka ni _____

8. Mtoto umleavyo _____

9. Mwana hutazama kisogo _____

10. Mtoto akibebwa halevyelevyi ______

Watu ambao hufanya kazi hizi huitwaje?
11. Hupaisha ndege-ulaya -

12. Huendesha gari-

13. Hutibu wagonjwa ____

14. Hufundisha watoto shuleni  -

15. Huuza maji mtaani kwa kutumia mkokoteni-

Bainisha NGELI ya maneno haya:
16.
Mkoba

17. Simba -

18. Shati -

19. Embe -

20. Mkuki -

ANDIKA WINGI WA NOMINO HIZI
21. Nyani -

22. Kobe -

23. Seremala -

24. Mtume -

25. Ndizi -

Andika majina ya matunda haya:

26. Wauzaji wa matunda ya nje ya Kenya Passion & Wauzaji - Bei nzuri za Soko

27.
Neema Herbalist & Nutrtional Foods Clinic: Faida ya juice za matunda mchanganyiko kama tiba y... | Papaya seeds, Seed salad, Papaya seed dressing recipe

28.
Matunda ya Xinjiang - china radio international

29.
FAIDA YA PARACHICHI KWA MWANAUME

30.
Ester Malibiche: FAHAMU FAIDA ZA KULA MATUNDA KWA UBORA WA AFYA YAKO

SHUGHULI YA 3:   KUSOMA NA KUFAHAMIKIWA.

Soma kifungu hiki kisha ujibu maswali.

        Mzee Ojwang' ni mzee mwenye bidii sana.Yeye hufanya kazi ya useremala. Katika karakana yake, yeye hutengeneza meza, makochi, na vifaa vingine. Yeye hupenda kuvaa bwelasuti ili nguo zake zisiwe chafu. Pia huvaa chepeo kuzuia ukali wa miale ya jua. Ameijenga nyumba yake upande wa kusini mwa shule ya Jahari. Nyumba hiyo ina vyumba kama vile sebule, maliwato, jikoni na vyumba vya kulala. Kila jioni Mzee Ojwang' na familia yake; watoto wawili na mke mmoja hukutana ili kula. Chakula hicho huwa kitamu kama asali. Kila mmoja hunawa kwa maji safi na sabuni kabla ya kula. Watoto husubiri wazazi wanawe kwanza ndipo nao wanawe.    Kila mtu hunyamaza akila. Wanaelewa kuwa kuongea na chakula mdomoni ni tabia mbaya. Baada ya kula, wote hunawa.Watoto huondoa vyombo mezani kisha wakamsaidia mama yao kuviosha. Baadaye wao huenda vitandani na kulala fofofo.

MASWALI.
1. Kazi ya Mzee Ojwang' ni ya kutengeneza vitu akitumia______

2. Vifaa atengezazo mzee Ojwang' kama vile meza, makabati, vitabu kwa ujumla huitwa

3. Ni nguo gani mzee Ojwang' huvaa ajikinge na uchafu akifanya kazi?

4. Shule ya Jahari iko upande gani kutoka kwa mzee Ojwang'?

5. Familia ya mzee Ojwang ni ya watu wangapi?

6. Chakula ambacho familia ya mzee Ojwang' hula jioni huitwaje?

7. Maliwato ni chumba cha kazi gani?

8. Tabia nzuri ambayo watoto wa mzee Ojwang huwa nayo wakila chakula ni ____

9. Kulala fo fo fo ni mfano wa ___

10. Chagua sentensi sahihi kati ya hizi:

2 Comments

  1. Grace Kiarie says:

    I seriously need revision materials for grade 4 and answers.Am not a Kiswahili Tr but due to the shortage of trs in school, Imebidi tu.
    Kindly help.Thanks in advance

  2. Margaret Maina says:

    Shukrani. Maswali haya yasaidia wanafunzi kudurusu.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WeCreativez WhatsApp Support
One of our Teachers is here. Ask for help
Hi, how can I help