Welcome to your GREDI YA 4 KISWAHILI. 2024 MID-TERM 2
ZIADA YA LIVU FUPI, KATI YA MUHULA WA 2 2024, GREDI YA 4.ZIADA YA WAKATI HUU ITAHUSU SHUGHULI ZA KISWAHILI.
2. Ndege wakiruka huwa wana_____ mtini.
3. Muhula ukimalizika wanafunzi hupewa _____ wakapumzike.
4. Wanafunzi wote lazima wavae _____ wakiwa shuleni.
5. Mwalimu wetu hupendeza sana kwa sababu yeye huvalia ______
6. Si vizuri wazazi ______ mtoto, ataharibika.
7. Mtu aki_______ na kijiti anaweza kutoka damu.
8. Mama alipoenda sokoni alinunua:maembe, machungwa, mboga, matofaa na _____
9. Ni ______ kubwa kukosa kumrekebisha mtoto akikosea.
10. Rafiki yako akija kwenu, ni vizuri _____ anapoenda.
11. Shairi ulilosikiliza lina beti ngapi?
12. Vina vya kati na mwisho katika ubeti wa tatu ni _______, ________
13. Mshororo 'Kubembea kuna mambo, kubembea tunacheza' unaitwaje?____
14. "Ng'riiiiiiiiii, sasa imelizwa'. Ni nini hiyo mshairi anasema?
15. Malenga wa shairi hili ni nani?
SHUGHULI YA 2 : MATUMIZI YA LUGHAJibu kila swali kulingana na maagizo yake.Toa majibu ya salamu hizi:1. Hamjambo - ______
2. Shikamoo-______
3. Salaam aleikum - ______
Jibu vitendawili hivi:4. Huku ng'o na kule ng'o _____________
5. Mama nieleke ______
6. Kuku wangu hutagia mibani ________
Kamilisha methali hizi:7. Mtoto wa nyoka ni _____
8. Mtoto umleavyo _____
9. Mwana hutazama kisogo _____
10. Mtoto akibebwa halevyelevyi ______
Watu ambao hufanya kazi hizi huitwaje?11. Hupaisha ndege-ulaya -
12. Huendesha gari-
13. Hutibu wagonjwa ____
14. Hufundisha watoto shuleni -
15. Huuza maji mtaani kwa kutumia mkokoteni-
Bainisha NGELI ya maneno haya:16. Mkoba
17. Simba -
18. Shati -
19. Embe -
20. Mkuki -
ANDIKA WINGI WA NOMINO HIZI21. Nyani -
22. Kobe -
23. Seremala -
24. Mtume -
25. Ndizi -
Andika majina ya matunda haya:26.
27.
28.
29.
30.
SHUGHULI YA 3: KUSOMA NA KUFAHAMIKIWA.Soma kifungu hiki kisha ujibu maswali.
Mzee Ojwang' ni mzee mwenye bidii sana.Yeye hufanya kazi ya useremala. Katika karakana yake, yeye hutengeneza meza, makochi, na vifaa vingine. Yeye hupenda kuvaa bwelasuti ili nguo zake zisiwe chafu. Pia huvaa chepeo kuzuia ukali wa miale ya jua. Ameijenga nyumba yake upande wa kusini mwa shule ya Jahari. Nyumba hiyo ina vyumba kama vile sebule, maliwato, jikoni na vyumba vya kulala. Kila jioni Mzee Ojwang' na familia yake; watoto wawili na mke mmoja hukutana ili kula. Chakula hicho huwa kitamu kama asali. Kila mmoja hunawa kwa maji safi na sabuni kabla ya kula. Watoto husubiri wazazi wanawe kwanza ndipo nao wanawe. Kila mtu hunyamaza akila. Wanaelewa kuwa kuongea na chakula mdomoni ni tabia mbaya. Baada ya kula, wote hunawa.Watoto huondoa vyombo mezani kisha wakamsaidia mama yao kuviosha. Baadaye wao huenda vitandani na kulala fofofo. MASWALI.1. Kazi ya Mzee Ojwang' ni ya kutengeneza vitu akitumia______
2. Vifaa atengezazo mzee Ojwang' kama vile meza, makabati, vitabu kwa ujumla huitwa
3. Ni nguo gani mzee Ojwang' huvaa ajikinge na uchafu akifanya kazi?
4. Shule ya Jahari iko upande gani kutoka kwa mzee Ojwang'?
5. Familia ya mzee Ojwang ni ya watu wangapi?
6. Chakula ambacho familia ya mzee Ojwang' hula jioni huitwaje?
7. Maliwato ni chumba cha kazi gani?
8. Tabia nzuri ambayo watoto wa mzee Ojwang huwa nayo wakila chakula ni ____
9. Kulala fo fo fo ni mfano wa ___
10. Chagua sentensi sahihi kati ya hizi:
Time's up
I seriously need revision materials for grade 4 and answers.Am not a Kiswahili Tr but due to the shortage of trs in school, Imebidi tu. Kindly help.Thanks in advance
Shukrani. Maswali haya yasaidia wanafunzi kudurusu.
Your email address will not be published. Required fields are marked *
Comment *
Name *
Email *
Website
Save my name, email, and website in this browser for the next time I comment.
Δ
2 Comments
I seriously need revision materials for grade 4 and answers.Am not a Kiswahili Tr but due to the shortage of trs in school, Imebidi tu.
Kindly help.Thanks in advance
Shukrani. Maswali haya yasaidia wanafunzi kudurusu.