KISWAHILI DARASA LA 7April 9, 2021GREDI YA 5, T1 KISWAHILI 2023.April 10, 2021 1 GREDI YA 4 KISWAHILI. 2024 MID-TERM 2 Welcome to your GREDI YA 4 KISWAHILI. 2024 MID-TERM 2 Name Class Phone Number ZIADA YA LIVU FUPI, KATI YA MUHULA WA 2 2024, GREDI YA 4.ZIADA YA WAKATI HUU ITAHUSU SHUGHULI ZA KISWAHILI. SHUGHULI ZA KISWAHILI MAAGIZO1. Fanya kazi yako katika MTANDAO kisha uiandike katika DAFTARI lako la kazi ya ziada.2. Ukimaliza kufanya kazi MTANDAONI, hapo chini utaona kitufe cha kukabidhi kazi kilichoandikwa 'Submit'. Bofya na baada ya sekunde kazi yako itakuwa imesahihishwa. Tazama matokeo na ufanye marudio ya maswali uliyonoa.3. Kumbuka utahitaji kuleta kazi iliyofanya daftarini shuleni, shule itakapofunguliwa.SHUGHULI YA 1: KUSIKILIZA NA KUONGEASikiliza kanda hii ya video kwa makini. https://jasipaschool.com/wp-content/uploads/2021/04/BEMBEA.mp4Tumia kamusi yako kutafuta maana ya maneno haya yaliyotumiwa katika shairi. bembea tatizo likizo tua kadhalika nadhifu dhaifu sare kwaruza sindikiza dekeza Sasa jibu maswali haya:1. Kibao kilichoning'inizwa kwa kamba mbili zilizofungiwa juu kwa ajili ya kuchezea huitwa_______ bembea jugwe tua None 2. Ndege wakiruka huwa wana_____ mtini. tua poa boa None 3. Muhula ukimalizika wanafunzi hupewa _____ wakapumzike. nadhifu likizo sare None 4. Wanafunzi wote lazima wavae _____ wakiwa shuleni. surupwenye dhaifu sare None 5. Mwalimu wetu hupendeza sana kwa sababu yeye huvalia ______ dhaifu nadhifu ovyo None 6. Si vizuri wazazi ______ mtoto, ataharibika. kumchapa kumdekeza kumlilia None 7. Mtu aki_______ na kijiti anaweza kutoka damu. kwaruzwa akisindikizwa sukumwa None 8. Mama alipoenda sokoni alinunua:maembe, machungwa, mboga, matofaa na _____ dhaifu kadhalika tua None 9. Ni ______ kubwa kukosa kumrekebisha mtoto akikosea. furaha raha tatizo None 10. Rafiki yako akija kwenu, ni vizuri _____ anapoenda. kumpiga kumsindikiza kumwambia asirudi None 11. Shairi ulilosikiliza lina beti ngapi? sita tano saba None 12. Vina vya kati na mwisho katika ubeti wa tatu ni _______, ________ ka, fu ka, ka ka, a None 13. Mshororo 'Kubembea kuna mambo, kubembea tunacheza' unaitwaje?____ mizani kibwagizo mwanzo None 14. "Ng'riiiiiiiiii, sasa imelizwa'. Ni nini hiyo mshairi anasema? baiskeli ndege kengele None 15. Malenga wa shairi hili ni nani? Mwalimu Wanto Mwalimu Omina Lucy Muthoni None SHUGHULI YA 2 : MATUMIZI YA LUGHAJibu kila swali kulingana na maagizo yake.Toa majibu ya salamu hizi:1. Hamjambo - ______ 2. Shikamoo-______ 3. Salaam aleikum - ______ Jibu vitendawili hivi:4. Huku ng'o na kule ng'o _____________ 5. Mama nieleke ______ 6. Kuku wangu hutagia mibani ________ nanasi None Kamilisha methali hizi:7. Mtoto wa nyoka ni _____ 8. Mtoto umleavyo _____ 9. Mwana hutazama kisogo _____ 10. Mtoto akibebwa halevyelevyi ______ Watu ambao hufanya kazi hizi huitwaje?11. Hupaisha ndege-ulaya - 12. Huendesha gari- 13. Hutibu wagonjwa ____ 14. Hufundisha watoto shuleni - 15. Huuza maji mtaani kwa kutumia mkokoteni- Bainisha NGELI ya maneno haya:16. Mkoba 17. Simba - 18. Shati - 19. Embe - 20. Mkuki - ANDIKA WINGI WA NOMINO HIZI21. Nyani - 22. Kobe - 23. Seremala - 24. Mtume - 25. Ndizi - Andika majina ya matunda haya:26. 27. 28. 29. 30. SHUGHULI YA 3: KUSOMA NA KUFAHAMIKIWA.Soma kifungu hiki kisha ujibu maswali. Mzee Ojwang' ni mzee mwenye bidii sana.Yeye hufanya kazi ya useremala. Katika karakana yake, yeye hutengeneza meza, makochi, na vifaa vingine. Yeye hupenda kuvaa bwelasuti ili nguo zake zisiwe chafu. Pia huvaa chepeo kuzuia ukali wa miale ya jua. Ameijenga nyumba yake upande wa kusini mwa shule ya Jahari. Nyumba hiyo ina vyumba kama vile sebule, maliwato, jikoni na vyumba vya kulala. Kila jioni Mzee Ojwang' na familia yake; watoto wawili na mke mmoja hukutana ili kula. Chakula hicho huwa kitamu kama asali. Kila mmoja hunawa kwa maji safi na sabuni kabla ya kula. Watoto husubiri wazazi wanawe kwanza ndipo nao wanawe. Kila mtu hunyamaza akila. Wanaelewa kuwa kuongea na chakula mdomoni ni tabia mbaya. Baada ya kula, wote hunawa.Watoto huondoa vyombo mezani kisha wakamsaidia mama yao kuviosha. Baadaye wao huenda vitandani na kulala fofofo. MASWALI.1. Kazi ya Mzee Ojwang' ni ya kutengeneza vitu akitumia______ vyuma mbao mabati None 2. Vifaa atengezazo mzee Ojwang' kama vile meza, makabati, vitabu kwa ujumla huitwa vifaa vya nyumbani makochi samani None 3. Ni nguo gani mzee Ojwang' huvaa ajikinge na uchafu akifanya kazi? surupwenye aproni suti None 4. Shule ya Jahari iko upande gani kutoka kwa mzee Ojwang'? Kusini Kaskazini Mashariki None 5. Familia ya mzee Ojwang ni ya watu wangapi? watatu watano wanne None 6. Chakula ambacho familia ya mzee Ojwang' hula jioni huitwaje? chamcha chajio kishuka None 7. Maliwato ni chumba cha kazi gani? kuogea na kwenda haja kuweka vyakula ambavyo havijapikwa kulala None 8. Tabia nzuri ambayo watoto wa mzee Ojwang huwa nayo wakila chakula ni ____ kutabasamu kumaliza chakula fyu! kutoongea wakila None 9. Kulala fo fo fo ni mfano wa ___ methali vitendawili tanakali za sauti None 10. Chagua sentensi sahihi kati ya hizi: Kunawa ni kuosha kiungo cha mwili ilhali kuoga ni kuosha mwili wote. Kuoga ni kuosha kiungo cha mwili ilhali kunawa ni kuosha mwili wote Kunawa na kuoga ni maneno yenye maana sawa. None Time's up Wanto 1 Comment Grace Kiarie says: March 23, 2024 at 7:08 am I seriously need revision materials for grade 4 and answers.Am not a Kiswahili Tr but due to the shortage of trs in school, Imebidi tu. Kindly help.Thanks in advance Reply Leave a Reply Cancel replyYour email address will not be published. Required fields are marked *Comment * Name * Email * Website Save my name, email, and website in this browser for the next time I comment. Δ
1 Comment
I seriously need revision materials for grade 4 and answers.Am not a Kiswahili Tr but due to the shortage of trs in school, Imebidi tu.
Kindly help.Thanks in advance