STD 6 KISWAHILISeptember 24, 2020STD 7 MATHEMATICSOctober 3, 2020 1 STD 5 KISWAHILI Welcome to your STD 5 KISWAHILI Name Class Phone KISWAHILI DARASA LA TANO.KUSOMA NA KUJIBU MASWALI YA UFAHAMU.SOMA HADITHI HII KISHA UJIBU MASWALI. Hapo zamani za kale, sungura na fisi walikuwa marafiki wa kufa kuzikana. La sungura lilikuwa ndilo la fisi na la fisi lilikuwa ndilo la sungura. Urafiki wao ulikita mizizi mpaka ukaonewa wivu na wanyama wengine. Wanyama hawa walijulikana sana na upendo wao ukazidi kukua siku baada ya nyingine. Huenda tabia za wanyama hawa ndizo zilizowaweka pamoja. Sungura alikuwa mjanja sana na kwa sababu ya ujanja wake aliweza kwenda na kutafuta chakula kwa urahisi. Fisi kwa upande mwingine alikuwa mlaza damu na mlafi. Kwa hivyo alifurahia kukaa nyumbani na mkewe wakifanya kazi nyepesi tu. Siku moja, sungura alikashirishwa sana na tabia ya fisi ya kumuomba chakula kila mara. Akaamua kumfunza adabu. Akambambia waende madukani kuna chakula kingi cha bure. Fisi akafurahi sana. Wakaenda. Huko madukani, sungura alinunua pombe wakanywa. Kwa ajili ya ulafi wa fisi, alikunywa haraka hadi akalewa chakari! Walipokuwa wakienda nyumbani, sungura alimwambia fisi, "Leo nitampiga mke wangu hadi afe. Amekuwa akila chakula ananimalizia kila wakati!". Fisi naye akaone kweli hata mke wake amekuwa akimmalizia chakula. Akaamua angempiga. Walifika kwa sungura kwanza. Sungura akamwambia fisi akae hapo barabarani asikie jinsi atakavyompiga mkewe. Akaingia na kuchukua ngoma. Akaipiga huku akipiga kelele na matusi. Kumbe mke wake alikuwa amelala usingizi wa pono! Fisi aliposikia hivyo akakimbia kwake. Akamwamsha mkewe akampiga sana huku akimtukana. Akampiga na kumpiga mpaka akafa. MASWALI1. Wanyama wanaozungumziwa hapa mwanzoni walikuwa_______ 2. Sungura na fisi walikuwa marafiki wa kufa na kuuana wa kufa na kupona wakubwa sana None 3. Urafiki wao ulikita mizizi; yaani ______ ulimea mizizi ulishika sana ulikuwa mwepesi None 4. Wanyama wengine waliwaonea sungura na fisi wivu kwa sababu _____ walikuwa marafiki wa dhati walikuwa warembo sana walikuwa na chakula kingi None 5. Fisi alikuwa mlafi sana. Ulafi ni tabia gani? Ya kutaka kulia sana Ya kutaka kula sana Ya kutaka kulala sana None 6. Kulaza damu ni ______ kuwa mzembe kuwa mvumilivu kuwa mcheshi None 7. Fisi alilewa chakari haraka kwa sababu _____ hakuwa amekula kitu kabla ya kunywa pombe yake ilikuwa kali zaidi ya kubugia pombe kwa umero None 8. Ni kweli kusema kuwa.... sungura alimpiga mke wake sana fisi hakumpiga mke wake alipiga ngoma sungura alimdanganya fisi akampige mkewe None 9. Mke wa sungura alikuwa amelala usingizi wa pono. Usingizi wa poni ni ____ mzito wa usumbufu mwepesi None 10. Maoni ya mwandishi katika hadithi hii ni kuwa... Tukiitwa twende madukani tusikubali Tamaa na ulafi si huleta madhara makubwa. Mke wa fisi alikufa na akazikwa. None Time's up Wanto Leave a Reply Cancel replyYour email address will not be published. Required fields are marked *Comment * Name * Email * Website Save my name, email, and website in this browser for the next time I comment. Δ