GRADE 5 END YEAR 2024 MATHEMATICSNovember 16, 2020STD 6 SCIENCENovember 19, 2020 0 STD 6 KISWAHILI Welcome to your STD 6 KISWAHILI Name Class Phone KISWAHILI DARASA LA 6MADA: SARUFIMADA NDOGO: KIREJESHI AMBAKirejeshi amba hutumika pamoja na virejeshi vyo "O" kulingana na ngeli. Tazama mifano hii hapa chini. Mtoto ambaye amepika ni wako. Watoto ambao wamepita ni wenu Kisu ambacho kilipotea ni cha baba. Visu ambavyo vilipotea ni vya baba. Gari ambalo lilianguka limeondolewa Magari ambayo yalianguka yameondolewa. Chupa ambayo imevunjika isitiwe chai Chupa ambazo zimevunjika zisitiwe chai. SASA FANYA ZOEZI HILI UKITUMIA AMBA.1. Daktari ____________ atakutibu ametoka Ulaya. 2. Wanafunzi __________ hawatasoma vizuri watafeli mtihani. 3. Somo _______ napenda zaidi ni Kiswahili. 4. Vyombo __________ ni safi vimeoshwa na mama. 5. Nyumba _________ zimejengwa ni nzuri. 6. Ugonjwa ___________ unasumbua ni wa Covid-19. 7. Pahali _________ mimi hulala pamejengwa vizuri. 8. Kitabu ________ ninaandikia si changu. 9. Ugali ___________ ulipikwa na mama ni mtamu sana. 10. Simu ________ ambayo imenunuliwa na baba ni nzuri sana. Time's up Wanto Leave a Reply Cancel replyYour email address will not be published. Required fields are marked *Comment * Name * Email * Website Save my name, email, and website in this browser for the next time I comment. Δ