KISWAHILI 5..June 28, 2020KISWAHILI 8,,June 29, 2020 0 KISWAHILI GREDI YA 4 MWISHO WA MWAKA 2024 Welcome to your KISWAHILI GREDI YA 4 MWISHO WA MWAKA 2024 Name Class Phone Number SHUGHULI ZA KISWAHILI GREDI YA 4, MUHULA WA TATU.WANYAMAPORITazama pcha hii.1. Je, kuna mnyama yeyote unayemjua hapa? 2. Taja wanyama ambao ushawahi kuwaona kwa macho?3. Wanyama hawa hupatikana wapi?4. Kuna wanyama wengine ambao huwako hapa unaowajua?Huyu ni Simbamarara.Tazama wanyama wengine hapa zaidi.Mnyama huyu ni fisi Mnyama huyu ni kakakuona.Huyu huitwa ChuiHuyu huitwa Duma. Tazama tofauti zilizopo kati ya Chui na duma. Chui ana madoadoa makubwa, kichwa kikubwa na ni mnene. Duma naye ana madoadoa madogo, kichwa kidogo na macho yenye mistari kama analia na mwili mwembamba.Wanyamapori wengine.1. Ngiri - ana meno mawili yanayotokea nje. Pia huitwa nguruwemwitu.2. Mbwamwitu-mnyama wa jamii ya mbwa, mkali na mwenye masikio makubwa.3. Kicheche - mnyama mwenye mdomo mrefu anayekula kuku.4. Kuchakulo - mnyama mdogo anayefukua mahindi shambani na kula.5. Nungunungu - mnyama mwenye mishale mwilini ya kurushia wengine akijilinda.6. Mbuni - ndege mkubwa sana wa porini asiyeweza kuruka.SHUGHULI ZA NYUMBANI.Mwambie mzazi wako akusaidie kuwatambua wanyamapori zaidi kupitia kwa mtandao wa simu yake.JIBU MASWALI HAYA.1. Ndege mkubwa wa porini asiyeweza kuruka huitwa_____ Mbuni Flamingo None 2. Simba mwenye milia au mistari mwilini huitwa____ Chui simbamarara None 3. Mnyama mwenye mbio zaidi ya wote huitwa____ duma fisi None 4. Nguruwemwitu pia huitwa ______ chui ngiri None 5. Mnyama wa porini anayefanana na ng'ombe ni______ Simba Mbogo None 6. Mimi ni mnyamapori. Ninaishi majini. Mimi ni_____ Kiboko Kifaru None 7. Mnyama anayeitwa tumbili ni wa familia ya _____ fisi nyani None 8. Wanyamapori huhifadhiwa katika _____ maktaba mbuga None 9. Kati ya wanyama hawa ni yupi wa porini? kicheche jogoo None 10. Kuku anayekaa mwituni huitwaje? kanga kasuku None Tazama Video hii na uisikilize kwa makini kisha ujibu maswali yafuatayo. https://jasipaschool.com/wp-content/uploads/2021/08/Shujaa-wa-samaki-Hadithi-za-Kiswahili-Swahili-Fairy-Tales.mp4Tazama maana ya maneno haya katika kamusi. himaya hela vua ufuo kibwengo thamani bashasha kasri fikicha macho himili Tumia baadhi ya maneno haya kukamilisha sentensi hizi.11. Eneo linalotawaliwa na mfalme huitwa _____ 12. Makao ya mfalme huitwa _____ 13. Jina jingine la pesa ni ______ 14. Kutoa samaki majini ni ku___ 15. Mtu akiwa na furaha tunaweza pia kusema kuwa ana ___ 16. Sehemu yenye mchanga mwingi kando kando ya bahari huitwa ____ 17. Mtu akiamka asubuhi huwa anaya.......... macho yake ili aone vizuri 18. Kulingana na hadithi, Shujaa wa samaki alipata jiwe la bahati kutoka kwa nani? Lafu Toni Kibwengo Mfalme None 19. Shujaa wa samaki alikuwa akiishi katika kijiji kilichoitwa ___ Pasadena Chokaa Monako None 20. Binti yake mfalme aliitwaje? Lafu Monako Viola None 21. Ahadi ya mfalme kwa bintiye ilikuwa gani? Kuwa angempa pesa nyingi Kuwa harusi yake ingefanyiwa baharini Kuwa yule ambaye angemchekesha angemuoa None 22. Je, baada ya mfalme kukutana na Lafu, alipendelea amuoe binti yake? Sijui La Ndio None 23. Kulingana na wewe, Viola alimpenda Lafu? Labda Sidhani Ndio None 24. Mfalme aliahidi Lafu kumpa nini baada ya harusi kufanyika? Nusu ya himaye yake Basi kubwa la kampuni Kasri lake kubwa None 25. Je, hadithi hii ni kuhusu nini? Binti ya mfalme Lafu na Toni Kibwengo Ndoto ya ajabu None VITENDAWILIKamilisha vitendawili vifuatavyo.26. Achora lakini hajui achoracho .... kobe mwanafunzi konokono None 27. Dada yangu aoga nusu jiwe la mtoni kuku majini flamingo None 28. Nyumba yangu haina mlango... tanki yai nanasi None 29. Naingia baharini nikiibuka nina ndevu nyeupe.... mwiko wa ugali machicha unga None 30. Kiti changu cha dhahabu hakikaliwi na mtu.... Sofa mkeka moto None METHALIKamilisha methali hizi31. Haraka haraka .... huharakisha haina baraka ndio mwendo None 32. Polepole ya kobe..... si nzuri hufanya afikiwe na wengine humfikisha mbali None 33. Ukila na kipofu..... usimmalizie usimguse mkono ukule polepole None 34. Asiyekujua..... hakuthamini si wa kwenu ni mkorofi None 35. Adui.... mpige muache aende mpende None None VIKEMBE (Watoto wa wanyama)36. Mtoto wa paka huitwa..... kipaka kitungule kinyaunyau None 37. Mtoto wa mbwa huitwa .... kilebu kibwa kambwa None 38. Mtoto wa kuku huitwa.... kigunge kifaranga yai None 39. Ndama ni mtoto wa .... ng'ombe nguruwe kiroboto None 40. Kiyoyo ni mtoto wa ..... bata farasi ndovu None LIKIZO NJEMA. UWE NA SIKUKUU ZENYE FANAKA. None Time's up Wanto Leave a Reply Cancel replyYour email address will not be published. Required fields are marked *Comment * Name * Email * Website Save my name, email, and website in this browser for the next time I comment. Δ