Welcome to your KISWAHILI GREDI YA 4 MWISHO WA MWAKA 2024
SHUGHULI ZA KISWAHILI GREDI YA 4, MUHULA WA TATU.WANYAMAPORITazama pcha hii.1. Je, kuna mnyama yeyote unayemjua hapa? 2. Taja wanyama ambao ushawahi kuwaona kwa macho?3. Wanyama hawa hupatikana wapi?4. Kuna wanyama wengine ambao huwako hapa unaowajua?Huyu ni Simbamarara.Tazama wanyama wengine hapa zaidi.Mnyama huyu ni fisi Mnyama huyu ni kakakuona.Huyu huitwa ChuiHuyu huitwa Duma. Tazama tofauti zilizopo kati ya Chui na duma. Chui ana madoadoa makubwa, kichwa kikubwa na ni mnene. Duma naye ana madoadoa madogo, kichwa kidogo na macho yenye mistari kama analia na mwili mwembamba.Wanyamapori wengine.1. Ngiri - ana meno mawili yanayotokea nje. Pia huitwa nguruwemwitu.2. Mbwamwitu-mnyama wa jamii ya mbwa, mkali na mwenye masikio makubwa.3. Kicheche - mnyama mwenye mdomo mrefu anayekula kuku.4. Kuchakulo - mnyama mdogo anayefukua mahindi shambani na kula.5. Nungunungu - mnyama mwenye mishale mwilini ya kurushia wengine akijilinda.6. Mbuni - ndege mkubwa sana wa porini asiyeweza kuruka.SHUGHULI ZA NYUMBANI.Mwambie mzazi wako akusaidie kuwatambua wanyamapori zaidi kupitia kwa mtandao wa simu yake.JIBU MASWALI HAYA.1. Ndege mkubwa wa porini asiyeweza kuruka huitwa_____
2. Simba mwenye milia au mistari mwilini huitwa____
3. Mnyama mwenye mbio zaidi ya wote huitwa____
4. Nguruwemwitu pia huitwa ______
5. Mnyama wa porini anayefanana na ng'ombe ni______
6. Mimi ni mnyamapori. Ninaishi majini. Mimi ni_____
7. Mnyama anayeitwa tumbili ni wa familia ya _____
8. Wanyamapori huhifadhiwa katika _____
9. Kati ya wanyama hawa ni yupi wa porini?
10. Kuku anayekaa mwituni huitwaje?
Tazama Video hii na uisikilize kwa makini kisha ujibu maswali yafuatayo.
12. Makao ya mfalme huitwa _____
13. Jina jingine la pesa ni ______
14. Kutoa samaki majini ni ku___
15. Mtu akiwa na furaha tunaweza pia kusema kuwa ana ___
16. Sehemu yenye mchanga mwingi kando kando ya bahari huitwa ____
17. Mtu akiamka asubuhi huwa anaya.......... macho yake ili aone vizuri
18. Kulingana na hadithi, Shujaa wa samaki alipata jiwe la bahati kutoka kwa nani?
19. Shujaa wa samaki alikuwa akiishi katika kijiji kilichoitwa ___
20. Binti yake mfalme aliitwaje?
21. Ahadi ya mfalme kwa bintiye ilikuwa gani?
22. Je, baada ya mfalme kukutana na Lafu, alipendelea amuoe binti yake?
23. Kulingana na wewe, Viola alimpenda Lafu?
24. Mfalme aliahidi Lafu kumpa nini baada ya harusi kufanyika?
25. Je, hadithi hii ni kuhusu nini?
VITENDAWILIKamilisha vitendawili vifuatavyo.26. Achora lakini hajui achoracho ....
27. Dada yangu aoga nusu
28. Nyumba yangu haina mlango...
29. Naingia baharini nikiibuka nina ndevu nyeupe....
30. Kiti changu cha dhahabu hakikaliwi na mtu....
METHALIKamilisha methali hizi31. Haraka haraka ....
32. Polepole ya kobe.....
33. Ukila na kipofu.....
34. Asiyekujua.....
35. Adui....
VIKEMBE (Watoto wa wanyama)36. Mtoto wa paka huitwa.....
37. Mtoto wa mbwa huitwa ....
38. Mtoto wa kuku huitwa....
39. Ndama ni mtoto wa ....
40. Kiyoyo ni mtoto wa .....
LIKIZO NJEMA. UWE NA SIKUKUU ZENYE FANAKA.
Time's up
Your email address will not be published. Required fields are marked *
Comment *
Name *
Email *
Website
Save my name, email, and website in this browser for the next time I comment.
Δ