KISWAHILI DARASA LA 6

GREDI YA 5, T1 KISWAHILI 2023.
April 10, 2021
KISWAHILI GREDI YA 2 MWISHO WA MWAKA 2024
April 12, 2021

KISWAHILI DARASA LA 6

Welcome to your KISWAHILI DARASA LA 6 2021

KAZI YA ZIADA YA LIVU YA MWISHO WA MWAKA, 2021

KISWAHILI



MAAGIZO
1. Fanya kazi yako katika MTANDAO kisha uiandike katika DAFTARI lako la kazi ya ziada.
2. Ukimaliza kufanya kazi MTANDAONI, hapo chini utaona kitufe cha kukabidhi kazi kilichoandikwa 'Submit'. Bofya na baada ya sekunde kazi yako itakuwa imesahihishwa. Tazama matokeo na ufanye marudio ya maswali uliyonoa.
3. Kumbuka utahitaji kuleta kazi iliyofanya daftarini shuleni, shule itakapofunguliwa.

KUSOMA NA KUFAHAMIKIWA.
UFAHAMU

Kuna wakati, Abunuwasi aliamua kuwa mfuga mbuzi. Alinunua mbuzi wa kufuga huku akiwa na lengo la kujiongezea kipato chake pindi mbuzi huyo atapoanza kuzaa, ili awafuge wanambuzi wawe wengi na kumuwezesha kuwa mkwasi kuliko wote waliokuwepo katika mji ule..
      Siku moja Abunuwasi akipokuwa akimpeleka mbuzi wake malishoni, alikuta kiatu kimoja kizuri sana katikati ya njia. Alisimama na kukiangalia. Kiatu kilipendeza machoni mwake ila akasema “Kiatu hiki ni kizuri lakini mbona kipo kimoja tu?” Alitafuta kiatu cha pili pembezoni mwa njia ila hakukiona. Alipoona hawezi kuvaa kiatu kimoja, aliamua kukiacha palepale... .
        Abunuwasi akamchukua mbuzi wake na mbele kidogo akaona kile kiatu cha mguu wa pili. Abunuwasi alishangaa na akaona bora angekichukua kile cha mwanzo kwa sababu cha pili kimepatikana. Akamfunga mbuzi wake pale akarudi.
Aliporudi pale mwanzo kukitafuta kiatu alichokiacha awali, hakukikuta tena. Alijaribu kukitafuta lakini hakukiona. Basi akadhani kuna mtu amekiokota. Akarudi haraka alipomfunga mbuzi wake nako pia hakumkuta mbuzi wala kile kiatu kimoja. Mwisho akawa amemkosa mbuzi na viatu. Ndoto zote za Abunuwasi kupata utajiri zikaruka na akabaki na ufukara wake kwa sababu ya tamaa yake.

A. MSAMIATI.
Tumia kamusi yako kutafuta maana ya maneno haya:
  • abunuwasi
  • fuga
  • pindi
  • lengo
  • pato
  • mkwasi
  • malishoni
  • pembezoni
  • awali
  • fukara
  • tamaa

I) MASWALI.
1. Kulingana na aya ya kwanza____

2. Abunuwasi alimnunua mbuzi akiwa na nia ya ______

3. Abunuwa alikiona kiatu _____

4. Kiatu alichokiona njiani....

5. Abuwasi alikitafuta kiatu cha pili wapi?

6. Je, abunuwasi aliamumua kufanya nini na kile kiatu cha kwanza?

7. Maana ya neno pembezoni kama lilivyotumika katika kifungu ni ____

8. Ni nini kilimfanya Abunuwasi ashangae?

9. Kulingana na aya ya mwisho,......

10. Ni methali gani ambayo ingetumiwa kumwelimisha Abunuwasi?

II) Tumia maneno uliyotafuta katika kamusi kujalizia sentensi hizi.
i) Chepkoech ni ______ sana, akipewa deni huepuka kulipa.

ii) Baba anapenda kuwa______ ng'ombe wa maziwa sana.

iii)  ________ mwalimu wetu alipoingia darasani, sote tulisimama.

iv) Mtu akikataa kufanya kazi atakuwa ______ maishani.

v) ______ la kwenda shuleni ni kupata elimu.

vi) Mtu akifanya kazi akapata mali mengi anakuwa ____

vii) Wageni waliambiwa wasimame _____ mwa ofisi wamngoje meneja.

viii) Methali... ______ ilimwua fisi.

ix) Ng'ombe na mbuzi hupelekwa ______ kukipambazuka.

x) Kila mtu ni lazima afanye kazi ili ajipatie ______

B. MATUMIZI YA LUGHA
Jibu kila swali kulingana na maagizo yake.
1. Chagua neno ambalo ni kivumishi katika sentensi hii:
     Mwanafunzi mtiifu hupewa zawadi.

2. Andika milioni sita laki sita tisini na sita elfu na tisa kwa tarakimu.

3. Kutokana na nomino mlaji tutaunda kitenzi ____

4. Shuleni kwetu ni karibu na kwao. Karibu iliyotumika huitwa karibu ya ____

5. Wingi wa neno dada ni _____

6. Malipo ya usafiri katika chombo chochote huitwa____

7. Kikembe cha sungura ni kitungule, cha farasi ni ______

8. Nzumari ni ala ya muziki ambayo huchezwa kwa _____

9. Upande mmoja wa karatasi ya kitabu kilichopigwa chapa huitwa___

10. Ni neno lipi kati ya haya si kiungo cha chakula? pilipili, pilau, bizari, dania.

11. ________ ni mnyama wa porini anayefanana na mbuzi, pia ni sehemu ya juu ya nyumba.

12. Chagua kiungo cha mwili ambacho ni tofauti na vingine. (ulimi,ubongo,utosi,utumbo)

13. Kimelea ambaye hupatikana katika undu wa kuku huitwaje?

14. Mshitakiwa husimama wapi akiwa mahakamani? ____

15. Kati ya zana hizi za vita, ni ipi ya kale? (manati,bunduki,kifaru,bomu)

C. MTUNGO.
Chagua neno lililo bora zaidi kati ya manne uliyopewa hapo chini kujalizia nafasi zilizoachwa wazi.

Ugonjwa wa Covid-19 sasa ___i___ makali yake baada ya ___ii____ watu ___iii____ sana. Hata ___iv____, kuna watu ___v____ wangali wanafanya mchezo kwa ____vi____ maagizo yaliyotolewa na Wizara ya ____vii____ . Watu kama hawa wanafaa kuchukuliwa ____viii____ kali, watozwe ____ix____ kubwa au wafungwe _____x____ . Ni vizuri kufuata maagizo ___xi____ ambayo ni ____xii_____ mikono kila mara, kukaa umbali wa ____xiii_____ na kuvaa ____xiv____. Tusipofanya hivyo tutakuja kujuta kwani ____xv____.

i.

ii.

iii.

iv.

v.

vi.

vii.

viii.

ix.

x.

xi.

xii.

xii.

xiv.

xv.

Tukutane juma lijalo.

Kwa heri.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WeCreativez WhatsApp Support
One of our Teachers is here. Ask for help
Hi, how can I help