GREDI YA 5, T1 KISWAHILI 2023.April 10, 2021KISWAHILI GREDI YA 2 MWISHO WA MWAKA 2024April 12, 2021 0 KISWAHILI DARASA LA 6 Welcome to your KISWAHILI DARASA LA 6 2021 Name Class Phone KAZI YA ZIADA YA LIVU YA MWISHO WA MWAKA, 2021 KISWAHILI MAAGIZO1. Fanya kazi yako katika MTANDAO kisha uiandike katika DAFTARI lako la kazi ya ziada.2. Ukimaliza kufanya kazi MTANDAONI, hapo chini utaona kitufe cha kukabidhi kazi kilichoandikwa 'Submit'. Bofya na baada ya sekunde kazi yako itakuwa imesahihishwa. Tazama matokeo na ufanye marudio ya maswali uliyonoa.3. Kumbuka utahitaji kuleta kazi iliyofanya daftarini shuleni, shule itakapofunguliwa.KUSOMA NA KUFAHAMIKIWA.UFAHAMU Kuna wakati, Abunuwasi aliamua kuwa mfuga mbuzi. Alinunua mbuzi wa kufuga huku akiwa na lengo la kujiongezea kipato chake pindi mbuzi huyo atapoanza kuzaa, ili awafuge wanambuzi wawe wengi na kumuwezesha kuwa mkwasi kuliko wote waliokuwepo katika mji ule.. Siku moja Abunuwasi akipokuwa akimpeleka mbuzi wake malishoni, alikuta kiatu kimoja kizuri sana katikati ya njia. Alisimama na kukiangalia. Kiatu kilipendeza machoni mwake ila akasema “Kiatu hiki ni kizuri lakini mbona kipo kimoja tu?” Alitafuta kiatu cha pili pembezoni mwa njia ila hakukiona. Alipoona hawezi kuvaa kiatu kimoja, aliamua kukiacha palepale... . Abunuwasi akamchukua mbuzi wake na mbele kidogo akaona kile kiatu cha mguu wa pili. Abunuwasi alishangaa na akaona bora angekichukua kile cha mwanzo kwa sababu cha pili kimepatikana. Akamfunga mbuzi wake pale akarudi.Aliporudi pale mwanzo kukitafuta kiatu alichokiacha awali, hakukikuta tena. Alijaribu kukitafuta lakini hakukiona. Basi akadhani kuna mtu amekiokota. Akarudi haraka alipomfunga mbuzi wake nako pia hakumkuta mbuzi wala kile kiatu kimoja. Mwisho akawa amemkosa mbuzi na viatu. Ndoto zote za Abunuwasi kupata utajiri zikaruka na akabaki na ufukara wake kwa sababu ya tamaa yake.A. MSAMIATI.Tumia kamusi yako kutafuta maana ya maneno haya: abunuwasi fuga pindi lengo pato mkwasi malishoni pembezoni awali fukara tamaa I) MASWALI.1. Kulingana na aya ya kwanza____ Abunuwasi alikuwa ameamua kumfunga mbuzi Abunuwasi alita kuwa mkulima wa kufuga mbuzi Abunuwasi alikuwa akimfuga mbuzi None 2. Abunuwasi alimnunua mbuzi akiwa na nia ya ______ maziwa nyama utajiri None 3. Abunuwa alikiona kiatu _____ alipokuwa akienda kumlisha mbuzi alipokuwa akitoka kununua mbuzi alipokuwa akimpeleka mbuzi sokoni None 4. Kiatu alichokiona njiani.... kilikuwa kimewekwa hapo kama mtego kilikuwa kimepotea kilikuwa kimetupwa hapo na mtu None 5. Abuwasi alikitafuta kiatu cha pili wapi? katikati ya barabara kando ya barabara katika msitu uliokuwa pembeni None 6. Je, abunuwasi aliamumua kufanya nini na kile kiatu cha kwanza? kukiuza apate pesa kukiacha pale tu kwenda nacho ili akatafute cha pili None 7. Maana ya neno pembezoni kama lilivyotumika katika kifungu ni ____ kando ya katikati ya mbele ya None 8. Ni nini kilimfanya Abunuwasi ashangae? alikiona kiatu cha pili alisahau kiatu cha kwanza alishindwa amfunge mbuzi wake wapi None 9. Kulingana na aya ya mwisho,...... Abunuwasi aliibiwa mbuzi na kiatu chake Abunuwasi alipoteza viatu vyake viwili akabaki na mbuzi Abunuwasi alienda hasara ya vitu vyote None 10. Ni methali gani ambayo ingetumiwa kumwelimisha Abunuwasi? Ukila na kipofu usimguse mkono Mbuzi wa kupewa haangaliwi meno Tamaa mbele mauti nyuma None II) Tumia maneno uliyotafuta katika kamusi kujalizia sentensi hizi.i) Chepkoech ni ______ sana, akipewa deni huepuka kulipa. abunuwasi mfugaji mwizi None ii) Baba anapenda kuwa______ ng'ombe wa maziwa sana. kamua fuga pindi None iii) ________ mwalimu wetu alipoingia darasani, sote tulisimama. Pindi Fuga Lengo None iv) Mtu akikataa kufanya kazi atakuwa ______ maishani. fukara mkwasi malishoni None v) ______ la kwenda shuleni ni kupata elimu. pato lengo awali None vi) Mtu akifanya kazi akapata mali mengi anakuwa ____ mkwasi fukara Abunuwasi None vii) Wageni waliambiwa wasimame _____ mwa ofisi wamngoje meneja. awali pindi pembezoni None viii) Methali... ______ ilimwua fisi. abunuwasi tamaa awali None ix) Ng'ombe na mbuzi hupelekwa ______ kukipambazuka. pembezoni mafugani malishoni None x) Kila mtu ni lazima afanye kazi ili ajipatie ______ awali pato pindi None B. MATUMIZI YA LUGHAJibu kila swali kulingana na maagizo yake.1. Chagua neno ambalo ni kivumishi katika sentensi hii: Mwanafunzi mtiifu hupewa zawadi. 2. Andika milioni sita laki sita tisini na sita elfu na tisa kwa tarakimu. 3. Kutokana na nomino mlaji tutaunda kitenzi ____ 4. Shuleni kwetu ni karibu na kwao. Karibu iliyotumika huitwa karibu ya ____ 5. Wingi wa neno dada ni _____ 6. Malipo ya usafiri katika chombo chochote huitwa____ 7. Kikembe cha sungura ni kitungule, cha farasi ni ______ 8. Nzumari ni ala ya muziki ambayo huchezwa kwa _____ 9. Upande mmoja wa karatasi ya kitabu kilichopigwa chapa huitwa___ 10. Ni neno lipi kati ya haya si kiungo cha chakula? pilipili, pilau, bizari, dania. 11. ________ ni mnyama wa porini anayefanana na mbuzi, pia ni sehemu ya juu ya nyumba. 12. Chagua kiungo cha mwili ambacho ni tofauti na vingine. (ulimi,ubongo,utosi,utumbo) 13. Kimelea ambaye hupatikana katika undu wa kuku huitwaje? 14. Mshitakiwa husimama wapi akiwa mahakamani? ____ 15. Kati ya zana hizi za vita, ni ipi ya kale? (manati,bunduki,kifaru,bomu) C. MTUNGO.Chagua neno lililo bora zaidi kati ya manne uliyopewa hapo chini kujalizia nafasi zilizoachwa wazi.Ugonjwa wa Covid-19 sasa ___i___ makali yake baada ya ___ii____ watu ___iii____ sana. Hata ___iv____, kuna watu ___v____ wangali wanafanya mchezo kwa ____vi____ maagizo yaliyotolewa na Wizara ya ____vii____ . Watu kama hawa wanafaa kuchukuliwa ____viii____ kali, watozwe ____ix____ kubwa au wafungwe _____x____ . Ni vizuri kufuata maagizo ___xi____ ambayo ni ____xii_____ mikono kila mara, kukaa umbali wa ____xiii_____ na kuvaa ____xiv____. Tusipofanya hivyo tutakuja kujuta kwani ____xv____.i. umeonesha imeonesha limeonesha ulionesha None ii. kuwuwa kuuwa kuua kuwua None iii. mingi mengi nyingi wengi None iv. ivo ivyo hivo hivyo None v. ambao ambayo ambaye ambazo None vi. kutozingatia kuzingatia kutoitikia kuitikia None vii. Elimu Afya Maji Mazingira None viii. panga hatua masharti nguvu None ix. fidia faida fola faini None x. korokoroni rumande husunini kituoni None xi. iliyotolewa yaliyotolewa zilizotolewa kilivyotolewa None xii. kuoga kusanitaisa kuosha kunawa None xii. kilometa moja na nusu sentimeta moja na nusu yadi moja na nusu kilogramu moja na nusu None xiv. magunia barakoa buibui viatu None xv. pilipili usiyoila yakuwashiani mgaagaa na upwa hali wali mkavu majuto ni mjukuu huja kinyume mwenda pole hajikwai None Tukutane juma lijalo.Kwa heri. None Time's up Wanto Leave a Reply Cancel replyYour email address will not be published. Required fields are marked *Comment * Name * Email * Website Save my name, email, and website in this browser for the next time I comment. Δ